12. Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya;Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;
13. Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake,Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.
15. Likumbukeni agano lake milele,Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
16. Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka;
17. Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri,Na Israeli liwe agano la milele.
18. Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,Iwe urithi wenu mliopimiwa;
19. Mlipokuwa watu wawezao kuhesabiwa;Naam, watu wachache na wageni ndani yake.
20. Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa,Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
21. Hakumwacha mtu awaonee;Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao;
22. Akisema, Msiwaguse masihi wangu,Wala msiwadhuru nabii zangu.
23. Mwimbieni BWANA, nchi yote;Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
24. Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,Na watu wote habari za maajabu yake.
25. Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
26. Maana miungu yote ya watu si kitu;Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.
27. Heshima na adhama ziko mbele zake;Nguvu na furaha zipo mahali pake.
28. Mpeni BWANA, enyi jamaa za watu,Mpeni BWANA utukufu na nguvu.
29. Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;Leteni sadaka, mje mbele zake;Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu;