1 Nya. 15:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. wa wana wa Elsafani; Shemaya mkuu wao, na nduguze mia mbili;

9. wa wana wa Hebroni; Elieli mkuu wao, na nduguze themanini;

10. wa wana wa Uzieli; Aminadabu mkuu wao, na nduguze mia na kumi na wawili.

11. Tena, Daudi akawaita Sadoki na Abiathari makuhani, na hao Walawi, Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli, na Aminadabu,

12. akawaambia, Ninyi ni vichwa vya mbari za baba za Walawi; jitakaseni, ninyi na ndugu zenu, ili mlipandishe sanduku la BWANA, Mungu wa Israeli, mpaka mahali pale nilipoliwekea tayari.

13. Kwani kwa sababu ninyi hamkulichukua safari ya kwanza, BWANA, Mungu wetu, alitufurikia, kwa maana hatukumtafuta sawasawa na sheria.

14. Basi makuhani na Walawi wakajitakasa, ili wapate kulipandisha sanduku la BWANA, Mungu wa Israeli.

1 Nya. 15