3. Basi Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu, ili kulipandisha sanduku la BWANA, mpaka mahali pake alipoliwekea tayari.
4. Daudi akawakutanisha wana wa Haruni, na Walawi;
5. wa wana wa Kohathi; Urieli mkuu wao, na nduguze mia na ishirini;
6. wa wana wa Merari; Asaya mkuu wao, na nduguze mia mbili na ishirini;
7. wa wana wa Gershoni; Yoeli mkuu wao, na nduguze mia na thelathini;
8. wa wana wa Elsafani; Shemaya mkuu wao, na nduguze mia mbili;
9. wa wana wa Hebroni; Elieli mkuu wao, na nduguze themanini;
10. wa wana wa Uzieli; Aminadabu mkuu wao, na nduguze mia na kumi na wawili.
11. Tena, Daudi akawaita Sadoki na Abiathari makuhani, na hao Walawi, Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli, na Aminadabu,
12. akawaambia, Ninyi ni vichwa vya mbari za baba za Walawi; jitakaseni, ninyi na ndugu zenu, ili mlipandishe sanduku la BWANA, Mungu wa Israeli, mpaka mahali pale nilipoliwekea tayari.
13. Kwani kwa sababu ninyi hamkulichukua safari ya kwanza, BWANA, Mungu wetu, alitufurikia, kwa maana hatukumtafuta sawasawa na sheria.