1 Nya. 15:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. Ndipo Daudi akasema, Haimpasi mtu awaye yote kulichukua sanduku la Mungu, isipokuwa Walawi peke yao; kwa kuwa hao ndio aliowachagua BWANA, ili walichukue sanduku la Mungu, na kumtumikia daima.

3. Basi Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu, ili kulipandisha sanduku la BWANA, mpaka mahali pake alipoliwekea tayari.

4. Daudi akawakutanisha wana wa Haruni, na Walawi;

5. wa wana wa Kohathi; Urieli mkuu wao, na nduguze mia na ishirini;

6. wa wana wa Merari; Asaya mkuu wao, na nduguze mia mbili na ishirini;

1 Nya. 15