2. Walikuwa wenye kupinda upinde, nao walikuwa hodari wa kutumia mkono wa kuume na wa kushoto, kwa kutupa mawe ya teo, na kwa kupiga mishale ya upinde; walikuwa wa nduguze Sauli, wa Benyamini.
3. Mkubwa wao alikuwa Ahiezeri, kisha Yoashi, wana wa Shemaa Mgibeathi; na Yezieli, na Peleti, wana wa Azmawethi; na Beraka, na Yehu Mwanathothi;
4. na Ishmaya Mgibeoni, shujaa wa wale thelathini, naye alikuwa juu ya wale thelathini; na Yeremia, na Yahazieli, na Yohana, na Yozabadi Mgederathi;
5. Eluzai, na Yerimothi, na Bealia, na Shemaria, na Shefatia Mharufi;
6. Elkana, na Ishia, na Azaleli, na Yoezeri, na Yashobeamu, Wakora;
7. na Yoela, na Zebadia, wana wa Yerohamu, wa Gedori.
8. Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima;
9. Ezeri mkubwa wao, Obadia wa pili, Eliabu wa tatu;
10. Mishmana wa nne, Yeremia wa tano;
11. Atai wa sita, Elieli wa saba;
12. Yohana wa nane, Elzabadi wa kenda;
13. Yeremia wa kumi, Makbanai wa kumi na moja.
14. Hao wa wana wa Gadi walikuwa maakida wa jeshi, yeye aliyekuwa mdogo amelingana na mia, na yeye aliyekuwa mkuu, na elfu.