1 Nya. 12:1-12 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi hawa ndio wale waliomjia Daudi huko Siklagi, alipokuwa akijificha kwa ajili ya Sauli, mwana wa Kishi; nao walikuwamo miongoni mwa wale mashujaa, waliomsaidia vitani.

2. Walikuwa wenye kupinda upinde, nao walikuwa hodari wa kutumia mkono wa kuume na wa kushoto, kwa kutupa mawe ya teo, na kwa kupiga mishale ya upinde; walikuwa wa nduguze Sauli, wa Benyamini.

3. Mkubwa wao alikuwa Ahiezeri, kisha Yoashi, wana wa Shemaa Mgibeathi; na Yezieli, na Peleti, wana wa Azmawethi; na Beraka, na Yehu Mwanathothi;

4. na Ishmaya Mgibeoni, shujaa wa wale thelathini, naye alikuwa juu ya wale thelathini; na Yeremia, na Yahazieli, na Yohana, na Yozabadi Mgederathi;

5. Eluzai, na Yerimothi, na Bealia, na Shemaria, na Shefatia Mharufi;

6. Elkana, na Ishia, na Azaleli, na Yoezeri, na Yashobeamu, Wakora;

7. na Yoela, na Zebadia, wana wa Yerohamu, wa Gedori.

8. Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima;

9. Ezeri mkubwa wao, Obadia wa pili, Eliabu wa tatu;

10. Mishmana wa nne, Yeremia wa tano;

11. Atai wa sita, Elieli wa saba;

12. Yohana wa nane, Elzabadi wa kenda;

1 Nya. 12