1 Nya. 1:45-54 Swahili Union Version (SUV)

45. Yobabu akafa, naye Hushamu, wa nchi ya Watemani, akamiliki badala yake.

46. Hushamu akafa, naye Hadadi, mwana wa Bedadi, akamiliki badala yake, ambaye aliwapiga Midiani katika uwanja wa Moabu; na jina la mji wake ni Avithi.

47. Hadadi akafa, naye Samla, wa Masreka, akamiliki badala yake.

48. Samla akafa, naye Shauli, wa Rehobothi karibu na Mto, akamiliki badala yake.

49. Shauli akafa, naye Baal-Hanani, mwana wa Akbori, akamiliki badala yake.

50. Baal-Hanani akafa, naye Hadadi akamiliki badala yake; na jina la mji wake ni Pau; na jina la mkewe ni Mehetabeli, binti Matredi, binti Mezahabu.

51. Akafa Hadadi. Na hawa ndio majumbe wa Edomu; jumbe Timna, na jumbe Alva, na jumbe Yethethi;

52. na jumbe Oholibama, na jumbe Ela, na jumbe Pinoni;

53. na jumbe Kenazi, na jumbe Temani, na jumbe Mibsari;

54. na jumbe Magdieli, na jumbe Iramu. Hao ndio majumbe wa Edomu.

1 Nya. 1