1 Kor. 9:23-25 Swahili Union Version (SUV)

23. Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.

24. Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25. Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

1 Kor. 9