1 Kor. 7:20-24 Swahili Union Version (SUV)

20. Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa.

21. Je! Uliitwa u mtumwa? Usione ni vibaya lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia.

22. Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo.

23. Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu.

24. Ndugu zangu, kila mtu na akae mbele za Mungu katika hali iyo hiyo aliyoitwa nayo.

1 Kor. 7