1 Fal. 8:49-52 Swahili Union Version (SUV)

49. basi, uyasikie maombi yao na dua yao, huko mbinguni, makao yako, ukaitetee haki yao;

50. ukawasamehe watu wako waliokutenda dhambi, na makosa yao yote waliyokukosa; ukawape kuonewa huruma mbele yao waliowachukua mateka, ili wapate kuwahurumia.

51. Kwa kuwa ni watu wako, na urithi wako, uliowatoa katika Misri, toka katikati ya tanuu ya chuma.

52. Macho yako na yafumbuke, na kuielekea dua ya mtumwa wako, na dua za watu wako Israeli, ukawasikilize kila wakati watakapokulilia.

1 Fal. 8