1 Fal. 15:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Mwaka wa ishirini wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa alianza kutawala juu ya Yuda.

10. Akatawala miaka arobaini na mmoja huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka, binti Absalomu.

11. Basi, Asa akafanya yaliyo mema machoni pa Mungu, kama alivyofanya babaye Daudi.

12. Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake.

13. Hata na Maaka, mamaye, akamwondolea daraja yake asiwe malkia, kwa kuwa amefanya sanamu ya kuchukiza kwa Ashera; basi Asa akaikata sanamu yake akaiteketeza penye kijito cha Kidroni.

14. Lakini mahali pa juu hapakuondoshwa; ila moyo wake Asa ulikuwa mkamilifu kwa BWANA siku zake zote.

1 Fal. 15