Yeremia 51:48-58 Biblia Habari Njema (BHN)

48. Kisha mbingu, dunia na vyote vilivyomovitaimba kwa furaha kuhusu kuanguka kwa Babuloni,waangamizi watakapofika kutoka kaskazini kuushambulia.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

49. Babuloni umesababisha vifo duniani kote;sasa wenyewe utaangamizwa kwa mauaji ya Israeli.

50. “Nyinyi mlinusurika kifo,ondokeni sasa, wala msisitesite!Ingawa mko nchi ya mbali mkumbukeni Mwenyezi-Mungu,ukumbukeni pia mji wa Yerusalemu.

51. Mnasema: ‘Tumeaibishwa na kufadhaishwa;aibu imezifunika nyuso zetu,kwa sababu wageni wameingiakatika sehemu takatifu za nyumba ya Mwenyezi-Mungu.’

52. “Kwa hiyo, wakati unakuja,nasema mimi Mwenyezi-Mungu,ambapo nitaviadhibu vinyago vya Babuloni,na majeruhi watapiga kite katika nchi yake yote.

53. Ingawa Babuloni atapanda mpaka mbinguni,na kuziimarisha ngome zake ndefu,waangamizi watakuja kutoka kwangu kumvamia.2Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

54. “Sikiliza! Kilio kinasikika kutoka Babuloni!Kishindo cha maangamizi makubwakutoka nchi ya Wakaldayo!

55. Maana mimi Mwenyezi-Mungu naiangamiza Babuloni,na kuikomesha kelele yake kubwa.Adui ananguruma kama mawimbi ya maji mengi,sauti ya kishindo chao inaongezeka.

56. Naam, mwangamizi anaijia Babuloni;askari wake wametekwa,pinde zao zimevunjwavunjwa.Mimi Mwenyezi-Mungu ni Mungu mwenye kuadhibu,hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.

57. Nitawalewesha wakuu na wenye hekima wake,watawala wake, madiwani na askari wake;watalala usingizi wa milele wasiinuke tena.Nasema mimi mfalme ambaye jina langu ni Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.

58. “Mimi Mwenyezi-Mungu wa Majeshi nasema:Ukuta mpana wa Babuloniutabomolewa mpaka chini,na malango yake marefuyatateketezwa kwa moto.Watu wanafanya juhudi za bure,mataifa yanajichosha maana mwisho wao ni motoni!”

Yeremia 51