Yeremia 51:31-35 Biblia Habari Njema (BHN)

31. Tarishi baada ya tarishi wanapiga mbio,mjumbe mmoja anamfuata mjumbe mwingine,kumpasha habari mfalme wa Babulonikwamba mji wake umevamiwa kila upande.

32. Vivuko vya mto vimetekwa,ngome zimechomwa moto,askari wamekumbwa na hofu.

33. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi:“Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafakawakati unapotayarishwa.Lakini bado kidogo tu,wakati wa mavuno utaufikia.”

34. Mfalme Nebukadneza wa Babulonialiuharibu na kuuponda mji wa Yerusalemualiuacha kama chungu kitupu;aliumeza kama joka.Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri,akautupilia mbali kama matapishi.

35. Watu wa Yerusalemu na waseme:“Babuloni na ulipizwe ukatili uleule,tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu!Babuloni ipatilizwekwa umwagaji wa damu yetu.”

Yeremia 51