35. Nami nitamfutilia mbali kila mtu katika Moabu ambaye anatambikia vilimani na kumfukizia ubani mungu wake.
36. “Kwa hiyo, moyo wangu unaomboleza juu ya watu wa Moabu na watu wa Kir-heresi, kama mpiga zumari mazishini; maana hata mali yote waliyojipatia imeangamia.
37. Kila mtu amenyoa upara na ndevu zake. Wote wamejikatakata mikononi na viunoni wamevaa mavazi ya gunia.
38. Juu ya nyumba za Moabu na katika viwanja vyao hakuna kinachosikika ila tu maombolezo. Mimi nimemvunja Moabu kama chombo kisichotakiwa na mtu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
39. Tazama alivyovunjika! Tazama wanavyoomboleza! Ajabu jinsi Moabu alivyorudi nyuma kwa aibu! Moabu amekuwa kichekesho na kioja kwa jirani zake wote.”
40. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Tazama, taifa litaruka kasi kuivamia Moabu,kama tai aliyekunjua mabawa yake.
41. Miji yake itatekwa,ngome zitachukuliwa.Siku hiyo mioyo ya wanajeshi wa Moabu,itaogopa kama mwanamke anayejifungua.
42. Wamoabu wataangamizwa, wasiwe tena taifa,kwa sababu walijikweza dhidi ya Mwenyezi-Mungu.
43. Kitisho, mashimo na mtego,vinawasubiri enyi watu wa Moabu.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
44. Atakayetoroka kitishoatatumbukia shimoni;atakayetoka shimoniatanaswa mtegoni.Kwa maana nitaleta mambo hayo juu ya Moabu,katika mwaka wao wa adhabu.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.