8. Ewe uliye tumaini la Israeli,mwokozi wetu wakati wa taabu,utakuwaje kama mgeni nchini mwetu,kama msafiri alalaye usiku mmoja?
9. Utakuwaje kama mtu uliyechanganyikiwa,kama shujaa asiyeweza kusaidia mtu?Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, u pamoja nasi;sisi twaitwa kwa jina lako, usituache.”
10. Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya watu hawa:“Kweli wamependa sana kutangatanga,wala hawakujizuia;kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu siwapokei.Sasa nitayakumbuka makosa yao,na kuwaadhibu kwa dhambi zao.”
11. Mwenyezi-Mungu aliniambia hivi: “Usiwaombee watu hawa fanaka.