Yeremia 14:8-11 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Ewe uliye tumaini la Israeli,mwokozi wetu wakati wa taabu,utakuwaje kama mgeni nchini mwetu,kama msafiri alalaye usiku mmoja?

9. Utakuwaje kama mtu uliyechanganyikiwa,kama shujaa asiyeweza kusaidia mtu?Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, u pamoja nasi;sisi twaitwa kwa jina lako, usituache.”

10. Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya watu hawa:“Kweli wamependa sana kutangatanga,wala hawakujizuia;kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu siwapokei.Sasa nitayakumbuka makosa yao,na kuwaadhibu kwa dhambi zao.”

11. Mwenyezi-Mungu aliniambia hivi: “Usiwaombee watu hawa fanaka.

Yeremia 14