19. Ole wangu mimi Yerusalemu maana nimejeruhiwa!Jeraha langu ni baya sana!Lakini nilisema: “Hakika haya ni mateso,na sina budi kuyavumilia.”
20. Lakini hema langu limebomolewa,kamba zake zote zimekatika;watoto wangu wameniacha, na kwenda zao,wala hawapo tena;hakuna wa kunisimikia tena hema langu,wala wa kunitundikia mapazia yangu.
21. Nami Yeremia nikasema:Wachungaji wamekuwa wajinga,hawakuomba shauri kwa Mwenyezi-Mungu;kwa sababu hiyo, hawakufanikiwa,na kondoo wao wote wametawanyika.