Sefania 1:16-18 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Siku hiyo ni ya mlio wa tarumbeta ya vita,dhidi ya miji yenye ngome na kuta ndefu.

17. Kwa kuwa watu wamemkosea Mwenyezi-Mungu,yeye atawaletea dhiki kubwa,hivyo kwamba watatembea kama vipofu.Damu yao itamwagwa kama vumbi,na miili yao kama mavi.

18. Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoakatika siku hiyo ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.Kwa moto wa wivu wakedunia yote itateketezwa.Kwa ukamilifu na kwa namna ya kutishaatawafanya wakazi wote duniani watoweke.

Sefania 1