1. Hii ndiyo baraka ambayo Mose, mtu wa Mungu aliwatakia Waisraeli kabla ya kufariki kwake. Alisema:
2. Mwenyezi-Mungu alikuja kutoka mlima Sinai,alitutokea kutoka mlima Seiri;aliiangaza kutoka mlima Parani.Alitokea kati ya maelfu ya malaika,na moto uwakao katika mkono wake wa kulia.