Isaya 57:17-21 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao;niliwaadhibu, nikauficha uso wangu na kukasirika.Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.

18. Niliiona mienendo yao, lakini nitawaponya;nitawaongoza na kuwapa faraja,nitawatuliza hao wanaoomboleza.

19. Mimi nitawapa amani,amani kwa walio mbali na walio karibu!Mimi nitawaponya.

20. Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka,ambayo haiwezi kutulia;mawimbi yake hutupa tope na takataka.”

21. Mungu wangu asema hivi:“Watu waovu sitawapa amani.”

Isaya 57