3. maana utapanuka kila upande;wazawa wako watamiliki mataifa,miji iliyokuwa mahame itajaa watu.
4. Usiogope maana hutaaibishwa tena;usifadhaike maana hutadharauliwa tena.Utaisahau aibu ya ujana wako,wala hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.
5. Muumba wako atakuwa mume wako;Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ndilo jina lake,Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako;yeye aitwa ‘Mungu wa ulimwengu wote’.
6. “Yerusalemu, Mwenyezi-Mungu amekuita tena wewekama vile mke aliyeachwa na kuhuzunika,mke aliyeolewa akiwa kijana akaachwa.Mungu wako anasema:
7. Nilikuacha kwa muda mfupi tu;kwa huruma nyingi, nitakurudisha.
8. Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa kitambo,lakini kwa fadhili za milele nitakuonea huruma.Mimi Mwenyezi-Mungu Mkombozi wako, nimesema.
9. “Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa:Wakati ule niliapa kwambasitaifunika tena ardhi kwa gharika.Basi sasa naapa kwamba sitakukasirikia tenawala sitakukemea tena.