8. “Sikiliza ewe Israeli, mtumishi wangu,wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua,wewe mzawa wa Abrahamu, rafiki yangu;
9. wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia,wewe niliyekuambia: ‘Wewe u mtumishi wangu;mimi sikukutupa, bali nilikuchagua.’
10. Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe.Usifadhaike, mimi ni Mungu wako.Nitakuimarisha na kukusaidia;nitakulinda kwa mkono wangu wa ushindi.
11. “Naam! Wote waliokuwakia hasira,wataaibishwa na kupata fedheha.Wote wanaopingana nawe,watakuwa si kitu na kuangamia.