12. Wako wapi, ewe Farao, wataalamu wako?Waache basi wakuambie na kukujulishaaliyopanga Mwenyezi-Mungu wa majeshi dhidi ya Misri!
13. Lakini viongozi wa Soani ni wapumbavu,wakuu wa Memfisi wamedanganyika.Hao walio msingi wa makabila yaowamelipotosha taifa la Misri.
14. Mwenyezi-Mungu amewamwagia hali ya vurugu,wakawapotosha Wamisri katika mipango yao yote,wakawa kama mlevi anayeyumbayumba akitapika.
15. Hakuna mtu yeyote nchini Misri,kiongozi au raia, mashuhuri au duni,awezaye kufanya lolote la maana.
16. Siku ile watu wa Misri wataogopa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu watakapomwona Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameunyosha mkono wake dhidi yao.