29. Kutoka Mithka, walipiga kambi yao Hashmona.
30. Kutoka Hashmona, walipiga kambi yao Moserothi.
31. Kutoka Moserothi, walipiga kambi yao Bene-yaakani.
32. Kutoka Bene-yaakani, walipiga kambi yao Hor-hagidgadi.
33. Kutoka Hor-hagidgadi, walipiga kambi yao Yot-batha.
34. Kutoka Yot-batha, walipiga kambi yao Abrona.
35. Kutoka Abrona, walipiga kambi yao Esion-geberi.
36. Waliondoka Esion-geberi, wakasafiri na kupiga kambi yao katika jangwa la Sini, (yaani Kadeshi).
37. Kutoka Kadeshi, walipiga kambi yao mlimani Hori, mpakani mwa nchi ya Edomu.
38. Kwa agizo la Mwenyezi-Mungu kuhani Aroni alipanda juu ya Mlima Hori, na huko, akafariki mnamo siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arubaini tangu Waisraeli walipotoka nchini Misri.