Ezekieli 29:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Wewe mtu! Mgeukie Farao mfalme wa Misri, utoe unabii juu yake na nchi yote ya Misri.

3. Mwambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Mimi nitapambana na wewe mfalme wa Misri,wewe mamba ulalaye mtoni Nili!Wewe unafikiri kwamba Nili ni wako,kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!

4. Basi, nitakutia ndoana tayani mwako,na kufanya samaki wakwame magambani mwako.Nitakuvua kutoka huko mtoni.

Ezekieli 29