Zek. 5:9-11 Swahili Union Version (SUV)

9. Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu.

10. Ndipo nikamwambia yule malaika aliyesema nami, Hawa wanaipeleka wapi efa hii?

11. Akaniambia, Wanakwenda kumjengea nyumba katika nchi ya Shinari; tena ikiisha kutengenezwa, atawekwa huko mahali pake mwenyewe.

Zek. 5