Zab. 94:4-11 Swahili Union Version (SUV)

4. Je! Wote watendao uovu watatoa maneno,Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?

5. Ee BWANA, wanawaseta watu wako;Wanautesa urithi wako;

6. Wanamwua mjane na mgeni;Wanawafisha yatima.

7. Nao husema, BWANA haoni;Mungu wa Yakobo hafikiri.

8. Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini;Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?

9. Aliyelitia sikio mahali pake asisikie?Aliyelifanya jicho asione?

10. Awaadibuye mataifa asikemee?Amfundishaye mwanadamu asijue?

11. BWANA anajua mawazo ya mwanadamu,Ya kuwa ni ubatili.

Zab. 94