3. BWANA, hata lini wasio haki,Hata lini wasio haki watashangilia?
4. Je! Wote watendao uovu watatoa maneno,Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?
5. Ee BWANA, wanawaseta watu wako;Wanautesa urithi wako;
6. Wanamwua mjane na mgeni;Wanawafisha yatima.
7. Nao husema, BWANA haoni;Mungu wa Yakobo hafikiri.
8. Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini;Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?