11. BWANA anajua mawazo ya mwanadamu,Ya kuwa ni ubatili.
12. Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye,Na kumfundisha kwa sheria yako;
13. Upate kumstarehesha siku za mabaya,Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo.
14. Kwa kuwa BWANA hatawatupa watu wake,Wala hutauacha urithi wake,
15. Maana hukumu itairejea haki,Na wote walio wanyofu wa moyo wataifuata.