1. Ee BWANA, Mungu wa kisasi,Mungu wa kisasi, uangaze,
2. Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze,Uwape wenye kiburi stahili zao.
3. BWANA, hata lini wasio haki,Hata lini wasio haki watashangilia?
4. Je! Wote watendao uovu watatoa maneno,Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?
5. Ee BWANA, wanawaseta watu wako;Wanautesa urithi wako;