Zab. 94:1-10 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, Mungu wa kisasi,Mungu wa kisasi, uangaze,

2. Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze,Uwape wenye kiburi stahili zao.

3. BWANA, hata lini wasio haki,Hata lini wasio haki watashangilia?

4. Je! Wote watendao uovu watatoa maneno,Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?

5. Ee BWANA, wanawaseta watu wako;Wanautesa urithi wako;

6. Wanamwua mjane na mgeni;Wanawafisha yatima.

7. Nao husema, BWANA haoni;Mungu wa Yakobo hafikiri.

8. Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini;Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?

9. Aliyelitia sikio mahali pake asisikie?Aliyelifanya jicho asione?

10. Awaadibuye mataifa asikemee?Amfundishaye mwanadamu asijue?

Zab. 94