Zab. 91:8-15 Swahili Union Version (SUV)

8. Ila kwa macho yako utatazama,Na kuyaona malipo ya wasio haki.

9. Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.

10. Mabaya hayatakupata wewe,Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11. Kwa kuwa atakuagizia malaika zakeWakulinde katika njia zako zote.

12. Mikononi mwao watakuchukua,Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

13. Utawakanyaga simba na nyoka,Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.

14. Kwa kuwa amekaza kunipendaNitamwokoa; na kumweka palipo juu,Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15. Ataniita nami nitamwitikia;Nitakuwa pamoja naye taabuni,Nitamwokoa na kumtukuza;

Zab. 91