3. Wamrudisha mtu mavumbini,usemapo, Rudini, enyi wanadamu.
4. Maana miaka elfu machoni pakoNi kama siku ya jana ikiisha kupita,Na kama kesha la usiku.
5. Wawagharikisha, huwa kama usingizi,Asubuhi huwa kama majani yameayo.
6. Asubuhi yachipuka na kumea,Jioni yakatika na kukauka.
7. Maana tumetoweshwa kwa hasira yako,Na kwa ghadhabu yako tumefadhaishwa.