Zab. 90:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Wewe, Bwana, umekuwa makao yetu,Kizazi baada ya kizazi.

2. Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia,Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.

3. Wamrudisha mtu mavumbini,usemapo, Rudini, enyi wanadamu.

4. Maana miaka elfu machoni pakoNi kama siku ya jana ikiisha kupita,Na kama kesha la usiku.

5. Wawagharikisha, huwa kama usingizi,Asubuhi huwa kama majani yameayo.

6. Asubuhi yachipuka na kumea,Jioni yakatika na kukauka.

Zab. 90