Zab. 9:12-19 Swahili Union Version (SUV)

12. Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka,Hakukisahau kilio cha wanyonge.

13. Wewe, BWANA, unifadhili,Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia;Wewe uniinuaye katika malango ya mauti,

14. Ili nizisimulie sifa zako zote;Katika malango ya binti SayuniNitaufurahia wokovu wako.

15. Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya;Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao.

16. BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu;Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.

17. Wadhalimu watarejea kuzimu,Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.

18. Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima;Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.

19. BWANA, usimame, mwanadamu asipate nguvu,Mataifa wahukumiwe mbele zako.

Zab. 9