11. Mwimbieni BWANA akaaye Sayuni,Yatangazeni kati ya watu matendo yake.
12. Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka,Hakukisahau kilio cha wanyonge.
13. Wewe, BWANA, unifadhili,Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia;Wewe uniinuaye katika malango ya mauti,
14. Ili nizisimulie sifa zako zote;Katika malango ya binti SayuniNitaufurahia wokovu wako.
15. Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya;Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao.
16. BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu;Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.
17. Wadhalimu watarejea kuzimu,Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.
18. Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima;Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.
19. BWANA, usimame, mwanadamu asipate nguvu,Mataifa wahukumiwe mbele zako.