1. Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote;Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu;
2. Nitafurahi na kukushangilia Wewe;Nitaliimbia jina lako, Wewe Uliye juu.
3. Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma;Hujikwaa na kuangamia mbele zako.
4. Kwa maana umenifanyia hukumu na hakiUmeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.
5. Umewakemea mataifa;Na kumwangamiza mdhalimu;Umelifuta jina lao milele na milele;