Zab. 89:41-44 Swahili Union Version (SUV)

41. Wote wapitao njiani wanateka mali zake;Amekuwa laumu kwa jirani zake;

42. Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake;Umewafurahisha wote wanaomchukia.

43. Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake;Wala hukumsimamisha vitani.

44. Umeikomesha fahari yake;Kiti chake cha enzi umekitupa chini.

Zab. 89