40. Umeyabomoa maboma yake yote,Umezifanya ngome zake kuwa magofu.
41. Wote wapitao njiani wanateka mali zake;Amekuwa laumu kwa jirani zake;
42. Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake;Umewafurahisha wote wanaomchukia.
43. Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake;Wala hukumsimamisha vitani.
44. Umeikomesha fahari yake;Kiti chake cha enzi umekitupa chini.
45. Umezipunguza siku za ujana wake;Umemvika aibu.
46. Ee BWANA, hata lini? Utajificha hata milele?Ghadhabu yako itawaka kama moto?
47. Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu;Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!