Zab. 89:35-47 Swahili Union Version (SUV)

35. Neno moja nimeliapa kwa utakatifu wangu,Hakika sitamwambia Daudi uongo,

36. Wazao wake watadumu milele,Na kiti chake kitakuwa kama jua mbele zangu.

37. Kitathibitika milele kama mwezi;Shahidi aliye mbinguni mwaminifu.

38. Walakini Wewe umemtupa na kumkataa,Umemghadhibikia masihi wako.

39. Umechukizwa na agano la mtumishi wako,Umeinajisi taji yake na kuitupa chini.

40. Umeyabomoa maboma yake yote,Umezifanya ngome zake kuwa magofu.

41. Wote wapitao njiani wanateka mali zake;Amekuwa laumu kwa jirani zake;

42. Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake;Umewafurahisha wote wanaomchukia.

43. Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake;Wala hukumsimamisha vitani.

44. Umeikomesha fahari yake;Kiti chake cha enzi umekitupa chini.

45. Umezipunguza siku za ujana wake;Umemvika aibu.

46. Ee BWANA, hata lini? Utajificha hata milele?Ghadhabu yako itawaka kama moto?

47. Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu;Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!

Zab. 89