Zab. 89:31-41 Swahili Union Version (SUV)

31. Wakizihalifu amri zangu,Wasiyashike maagizo yangu,

32. Basi, nitawarudi makosa yao kwa fimbo,Na uovu wao kwa mapigo.

33. Lakini fadhili zangu sitamwondolea yeye,Wala sitafanya uaminifu wangu kuwa uongo.

34. Mimi sitalihalifu agano langu,Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu.

35. Neno moja nimeliapa kwa utakatifu wangu,Hakika sitamwambia Daudi uongo,

36. Wazao wake watadumu milele,Na kiti chake kitakuwa kama jua mbele zangu.

37. Kitathibitika milele kama mwezi;Shahidi aliye mbinguni mwaminifu.

38. Walakini Wewe umemtupa na kumkataa,Umemghadhibikia masihi wako.

39. Umechukizwa na agano la mtumishi wako,Umeinajisi taji yake na kuitupa chini.

40. Umeyabomoa maboma yake yote,Umezifanya ngome zake kuwa magofu.

41. Wote wapitao njiani wanateka mali zake;Amekuwa laumu kwa jirani zake;

Zab. 89