Zab. 89:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Nimefanya agano na mteule wangu,Nimemuapia Daudi, mtumishi wangu.

4. Wazao wako nitawafanya imara milele,Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele.

5. Ee BWANA, mbingu zitayasifu maajabu yako,Uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu.

6. Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na BWANA?Ni nani afananaye na BWANA miongoni mwa malaika?

7. Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu,Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

Zab. 89