1. Fadhili za BWANA nitaziimba milele;Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
2. Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako.
3. Nimefanya agano na mteule wangu,Nimemuapia Daudi, mtumishi wangu.
4. Wazao wako nitawafanya imara milele,Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele.
5. Ee BWANA, mbingu zitayasifu maajabu yako,Uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu.
6. Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na BWANA?Ni nani afananaye na BWANA miongoni mwa malaika?
7. Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu,Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
8. BWANA, Mungu wa majeshi,Ni nani aliye hodari kama Wewe, Ee YAHU?Na uaminifu wako unakuzunguka.
9. Wewe ndiwe ukitawalaye kiburi cha bahari.Mawimbi yake yainukapo wayatuliza Wewe.