Zab. 88:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Mimi umenilaza katika shimo la chini,Katika mahali penye giza vilindini.

7. Ghadhabu yako imenilemea,Umenitesa kwa mawimbi yako yote.

8. Wanijuao umewatenga nami;Umenifanya kuwa chukizo kwao;Nimefungwa wala siwezi kutoka.

9. Jicho langu limefifia kwa ajili ya matesoBWANA, nimekuita kila siku;Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.

10. Wafu je! Utawafanyia miujiza?Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?

Zab. 88