6. Mimi umenilaza katika shimo la chini,Katika mahali penye giza vilindini.
7. Ghadhabu yako imenilemea,Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
8. Wanijuao umewatenga nami;Umenifanya kuwa chukizo kwao;Nimefungwa wala siwezi kutoka.
9. Jicho langu limefifia kwa ajili ya matesoBWANA, nimekuita kila siku;Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.
10. Wafu je! Utawafanyia miujiza?Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?