10. Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu,Wewe ndiwe mfanya miujiza,Ndiwe Mungu peke yako.
11. Ee BWANA, unifundishe njia yako;Nitakwenda katika kweli yako;Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;
12. Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu,Kwa moyo wangu wote,Nitalitukuza jina lako milele.
13. Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana;Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu.
14. Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia;Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho.Wala hawakukuweka WeweMbele ya macho yao.
15. Lakini Wewe, Bwana,U Mungu wa rehema na neema,Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli.
16. Unielekee na kunifadhili mimi;Mpe mtumishi wako nguvu zako,Umwokoe mwana wa mjakazi wako.