Zab. 83:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee Mungu, usistarehe,Ee Mungu, usinyamae, wala usitulie.

2. Maana adui zako wanafanya ghasia,Nao wakuchukiao wameviinua vichwa vyao.

3. Juu ya watu wako wanafanya hila,Na kushauriana juu yao uliowaficha.

4. Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa,Na jina la Israeli halitakumbukwa tena.

5. Maana wanashauriana kwa moyo mmoja,Juu yako wanafanyana agano.

6. Hema za Edomu, na Waishmaeli,Na Moabu, na Wahagari,

Zab. 83