Zab. 81:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;

9. Usiwe na mungu mgeni ndani yako;Wala usimsujudie mungu mwingine.

10. Mimi ndimi BWANA, Mungu wako,Niliyekupandisha toka nchi ya Misri;Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.

11. Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,Wala Israeli hawakunitaka.

12. Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,Waenende katika mashauri yao.

Zab. 81