4. Kwa maana ni sheria kwa Israeli,Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5. Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu,Alipoondoka juu ya nchi ya Misri;Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
6. Nimelitenga bega lake na mzigo,Mikono yake ikaachana na kikapu.
7. Katika shida uliniita nikakuokoa;Nalikuitikia katika sitara ya radi;Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
8. Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;