Zab. 81:4-12 Swahili Union Version (SUV)

4. Kwa maana ni sheria kwa Israeli,Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.

5. Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu,Alipoondoka juu ya nchi ya Misri;Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.

6. Nimelitenga bega lake na mzigo,Mikono yake ikaachana na kikapu.

7. Katika shida uliniita nikakuokoa;Nalikuitikia katika sitara ya radi;Nalikujaribu penye maji ya Meriba.

8. Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;

9. Usiwe na mungu mgeni ndani yako;Wala usimsujudie mungu mwingine.

10. Mimi ndimi BWANA, Mungu wako,Niliyekupandisha toka nchi ya Misri;Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.

11. Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,Wala Israeli hawakunitaka.

12. Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,Waenende katika mashauri yao.

Zab. 81