2. Pazeni zaburi, pigeni matari,Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
3. Pigeni panda mwandamo wa mwezi,Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.
4. Kwa maana ni sheria kwa Israeli,Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.
5. Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu,Alipoondoka juu ya nchi ya Misri;Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.