Zab. 81:11-15 Swahili Union Version (SUV)

11. Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,Wala Israeli hawakunitaka.

12. Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,Waenende katika mashauri yao.

13. Laiti watu wangu wangenisikiliza,Na Israeli angeenenda katika njia zangu;

14. Ningewadhili adui zao kwa upesi,Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;

15. Wamchukiao BWANA wangenyenyekea mbele zake,Bali wakati wao ungedumu milele.

Zab. 81