11. Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,Wala Israeli hawakunitaka.
12. Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,Waenende katika mashauri yao.
13. Laiti watu wangu wangenisikiliza,Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
14. Ningewadhili adui zao kwa upesi,Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;
15. Wamchukiao BWANA wangenyenyekea mbele zake,Bali wakati wao ungedumu milele.